Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

2016 KCSE 4MCK Joint Exam

Kiswahili Paper 3

SEHEMU A: (Alama 20)

USHAIRI
1.

Maswali
a)Eleza dhamira ya shairi hili? (al. 2)
b)Kwa nini mtunzi anashidwa kumwamini mwanasiasa? (al.2)
c)Onyesha namna mtunzi ametumia idhini yake ya utunzi huku ukitoa mifano wafaka? (al. 4)
d)Bainisha toni ya shairi hili? (al. 2)

e)Jadili tamathali za usemi mbili alizotumia mwandishi kuwasilisha ujumbe wake? (al. 4)
f)Andika ubeti wa pili kwa lugha nadhari. (al.4)
g)Kwa kutoa ithibati , shairi hili ni aina gani? (al. 2)

20 marks

SEHEMU YA B: (Alama 20)

TAMTHILIA: Mstahiki Meya Timothy Arege. Mstahiki Meya
2.

Nanyi vile vile msikate tamaa. Endeleeni kushinikiza Meya. Mlango hatimaye huenda ukasalimu
amri.”
a)Eleza muktadha wa dondoo hili. (al. 4)
b)Huku ukitoa mifano, bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili. (al. 4)
c)Onyesha namna wanacheneo walivyojitahidi kuboresha hali zao. (al. 2)
AU

20 marks

3.

Eleza jinsi mbinu ya istiari ilivyotumika katika tamthilia ya mstahiki meya.

20 marks

SEHEMU YA C: (Alama 20)

Riwaya. Ken Walibora. KIDAGAA KIMEMWOZEA
4.

“Ujenzi wa jamii mpya ni jukumu la vijana.” Jadili kwa kurejelea riwaya hii.

20 marks

5.

’Hata haramu huhalalishwa, ati, ‘Haramu ngapi zimehalalishwa? Chungu nzima……”
a) Eleza muktasha wa dondoo hii. (al. 4)
b)Ni mbinu zipi za lugha zilizotumika katika kifungu hiki. (al 4)
c)Bainisha ukweli wa dondoo hili kwa kurejelea Riwaya nzima. (al. 12)

20 marks

SEHEMU YA D: (Alama 20)

HADITHI FUPI
6.

Mwanamke katika diwani ya Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine amepewa nafasi finyu.
Fafanua kwa kuzingatia hadithi zozote nne.

20 marks

7.

Tukio lililowaleta hapa ni la kawaida kwetu. Ingawa sisi hufanya tuwezayo kuwalinda wanetu, mara
nyingi tabia zao hutupiga chenga……….

a)Eleza muktadha wa dondoo hili. (al. 4)
b)Eleza sia nne za mzungumzaji. (al. 8)
c)Jadili matatizo manne yanayojitokeza katika hadithi hii. (al. 8)

20 marks

SEHEMU YA E: (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI
8.

i)Ngomezi ni nini? (al. 2)
ii)Jadili changamoto za ngomezi ya kimapokeo katika jamii ya sasa. (al. 8)
iii)Taja mifano miwili ya ngomezi za kisasa. (al. 2)
iv)Fafanua hasara zozote nne za miviga katika jamii. (al. 8)

20 marks

Back Top